Palestina ni nchi ya pekee upande wa jiografia, hasa upande wa mashariki, katika Bonde la Ufa unapotiririka mto Yordani hadi Bahari ya Chumvi.
Mipaka ya Palestina imebadilikabadilika katika historia.
Katika karne ya 5 KK Herodotus alipotaja Palaestina alifanya hivyo kwa maana tofauti kadiri ya mukhtada.[1]
Wapalestina wa leo wanataka mipaka yao iwe ile ya eneo lindwa lililokuwa chini ya Waingereza, yaani bila ya nchi ya Yordan, ng'ambo ya mto huo.[2]